Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimetoa ripoti ya robo mwaka ya hali ya uwekezaji nchini huku Tanzania ikionesha kushika nafasi ya tano miongoni mwa mataifa 10 duniani, ambayo uchumi wake unakua kwa kasi.
Akitoa ripoti hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TIC, Geofrey Mwambe alisema kuimarika kwa hali hiyo ya uchumi, kunatokana na uhamasishaji unaoendelea kufanywa na TIC kupitia njia mbalimbali ikiwemo mikutano ya ndani na nje ya nchi kuhamasisha uwekezaji.
Alisema katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Aprili, mwaka huu Kituo hicho kimefanikisha uandikishaji wa miradi mipya 109 yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 13.3 inayotarajiwa kutoa fursa za ajira 18,172 kwa wananchi mbalimbali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |