Mkurugenzi mkuu wa kongamano la mageuzi ya Afrika Rwanda Patrick Yoon amesema licha ya changamoto za hapa na pale katika kuafikia malengo yao,juhudi na ushirikiano na serikali ya Korea wamefikia walengwa na kuboresha biashara kupitia kwa teknolojia ya mtandao huo wa kasi.
Rwanda imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika kufikisha mtandao wa 4G katika mikoa yote .
Washikadau wa sekta ya mitandao na biashara nchini Rwanda wanasema nchi hiyo itaingia miongoni mwa nchi zitakazopata mabadiliko makuu ya viwanda kwa kuimarisha matumizi ya teknolojia.
Mtandao huo umechangia kubuni ajira na huduma mpya katika sekta ya mawasiliano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |