Dereva Lewis Hamilton ameendeleza rekodi ya kushinda baada ya kushika nafasi ya kwanza kwenye mashindano ya magari ya mwendokasi ya Barcelona jana nchini Hispania.
Katika mbio hizo, nafasi ya pili ilikwenda kwa dereva mwenzake wa Mercedes, Valterri Bottas wa Finland, na nafasi ya tatu ikichukuliwa na Max Verstappen wa Ubelgiji na timu ya Redbull.
Mpinzani wa Karibu wa Lewis, ambaye ni dereva wa Ferari, mjerumani Sebastian Vettel jana alishika nafasi ya 4.
Ushindi huu pamoja na ule aliopata Aprili 29 nchini Azerbaijan, unamuongezea alama muhimu kwa ajili ya kushinda ubingwa wa jumla kwenye mashindano hayo msimu huu.
Madereva hao sasa wanajiandaa na mashindano ya Monaco-Ufaransa, Mei 27.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |