Kampuni ya Dorae Inc ambayo inasaidia na teknolojia hiyo inasema lengo ni ni kuzuia madini yanayotoka kwenye maeneo yanayokumbwa na migogoro kuuzwa nje.
Dorae Inc, inafuatilia madini kama vile cobalt, coltan na almasi kutoka DRC.
Mpango huo utasaida serikali pia kwani ushuru unaolipwa utaongezeka kwa asilimia 2.
Nchini DRC madini ya Cobalt, coltan na almasi huchimbwa kinyume cha sheria kwenye eneo la mashariki na pesa za madini hayo kutumika kufadhili makundi ya wapiganaji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |