• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Tanzania yapiga hatua kubwa mradi wa bomba la mafuta

    (GMT+08:00) 2018-05-15 18:16:04

    Maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) kutoka Hoima, Uganda mpaka Bandari ya Tanga Tanzania, yako asilimia 80 kwa upande wa Tanzania.

    Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani amesema Tanzania iko mbele asilimia 80 katika maendeleo ya utekelezaji wa bomba la mafuta ghafi. Alisema kwa upande wa Uganda wako asilimia 20.

    Alisema mradi huo ulianza utekelezaji kwenye jiwe la msingi na sasa utekelezaji wake utaanza.

    Waziri Kalemani alisema tayari wamefanya mkutano wa tathimini na hatua zilizofikiwa kwa nchi mbili, ambapo mkutano huo uliwahusisha mawaziri akiwemo Waziri wa Nishati.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako