Baada ya timu ya taifa ya Rwanda kushika nafasi ya tatu kati ya timu kwenye mashindano ya awali ya Afrika ya mchezo wa Raga, wadau wa maendeleo ya mchezo huo wamelitupia lawama shirikisho la raga kitaifa RRF kwa kile wanachodai ni kutoifanyia maandalizi sahihi nay a kutosha timu hiyo.
Kutokana na lawama hizo, katibu mkuu wa RRF amewaambia waandishi wa habari kuwa, RRF inapokea maoni hayo, na kwamba jitihada kubwa zitafanyika ili kujitahidi kufanya vizuri.
Rwanda sasa imeondolewa katika michuano ya kufuzu kombe la dunia mwaka 2019, na imesaliwa na mashindano ya kufuzu michezo ya olimpiki mwaka 2020, ambapo itaanza kampeni zake mwezi Septemba mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |