Kocha mkuu wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola ametangazwa kuwa kocha bora wa msimu uliopita katika ligi kuu ya Uingereza, baada ya kuiwezesha klabu yake kushidna taji la ubingwa wa ligi ikiwa na rekodi nyingi ndani yake ikiwemo kufikisha pointi 100 na kupata ushindi mara 32 ndani ya msimu mmoja.
Katika kinyang'anyiro hicho msimu huu, Pep alikuwa anawania nafasi hiyo na makocha wengine sita ambao waling'ara pia akiwemo Jurgen Klopp (Liverpool), Sean Dyche (Burnley), Nuno Espirito Santo (Wolves), Neil Warnock (Cardiff) and John Coleman (Accrington Stanley).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |