Katika kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo unakuwa wa uhakika na kwa bei nafuu,imependekeza kufuta tozo tano kwenye uzalishaji mbegu huku ikipendekeza kufuta tozo zingine sita kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya ushirika.
Imeelezwa kuwa hatua hiyo ya serikali ni sehemu ya mkakati wa kumaliza kero zinazowakabili wakulima ambao Rais John Pombe Magufuli amekuwa akiusisitiza.
Kuhakikisha mkakati huo unatekelezwa,serikali imesema imefanya marekebisho ya kanuni na sheria zilizoanzisha tozo na ada husika,hivyo utekelezaji wake uzingatiwe na hatua kali zitachukuliwa kwa watakaokiuka.
Uuamuzi huo wa serikali ulitangazwa jana bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Kilimo ,Dk Charles Tizeba,alipowasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka ujao wa fedha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |