Klabu ya Atletico Madrid ya Hispania jana imeshinda ubingwa wa ligi ya Yuropa baada ya kuifunga magoli 3-0 timu ya Olympic Marseille kwenye mechi ya fainali iliyopigwa jana nchini Ufaransa.
Magoli ya Atletico yalifungwa na Antoinne Grizmann alyefunga mawili na moja likifungwa na Gabriel Fernandez 'Gabi'.
Ubingwa huu ni wa tatu kwa Atletico katika kipindi cha miaka mitatu, baada ya kushinda taji hilo pia mwaka 2010 na mwaka 2012.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |