Inaelezwa kuwa Arsenal watafanya mazungumzo na mchezaji wao zamani, Mikael Arteta wa Hispania kwa ajili ya kuchukua nafasi ya kocha iliyoachwa wazi na Arsene Wenger.
Arteta mwenye miaka 36 sasa, ni kocha msaidizi wa klabu ya Manchester City inayofundishwa na Pep Guardiola, na endapo makubaliano yatafikiwa, atapata dau la pauni milioni 50 msimu huu.
Mazungumzo hayo muhimu yataongozwa na mkurugenzi mkuu wa Arsenal Ivan Gazidis, mkuu wa idara ya maendeleo ya soka Raul Sanllehi na mkuu wa kitengo cha usajili Sven Mislintat.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |