Mchezaji nyota wa mchezo wa mpira wa magongo (baseball) anayeshiriki ligi kuu ya kulipwa nchini Marekani akiwa na timu ya Seattle Mariners, Robinson Cano ambaye ni raia wa Jamhuri ya Dominica amefungiwa kutoshiriki michezo 80 kutokana na hatia ya kutumia dawa zilizopigwa marufuku kwa wanamichezo.
Vipimo vilionyesha kuwa mchezaji huyo alitumia dawa aina ya diuretic Furosemide, ambapo yeye mwenyewe alikiri kutumia akiwa likizo nchini Dominica, lakini pasipo kujua kuwa zimepigwa marufuku, hivyo ameomba radhi mashabiki na uongozi wa timu ambao umeleeza kushtushwa na taarifa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |