Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye amesema chanzo cha kufungwa kwa biashara nyingi nchini ni mazingira magumu ya biashara na sera kandamizi zilizopo.
Simbeye alisema utafiti uliofanywa na TPSF umebaini kuwa biashara 4,640 zimefungwa nchini katika cha miaka mitatu.Alisema Tanzania inatakiwa kupiga hatua zaidi katika suala la ujasiriamali, kwa kuwa sasa ni sekta pekee inayozalisha ajira kwa wingi nchini.Pia, mkurugenzi huyo alisema uchumi wa viwanda kwa Tanzania kwa nchi za Afrika Mashariki, bado upo chini ukilinganisha na Kenya ambayo ina viwanda 500,000 wakati Tanzania ina 53,876.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |