Nchini Tanzania, mtendaji mkuu wa bodi ya ligi za soka Boniface Wambura jana alifika mahakamani mjini Dar es Salaam kutoa ushahidi kwenye kesi inayomkabili rais wa zamani wa shirikisho la mpira wa miguu TFF, Jamal Malinzi na wenzake wanne.
Mahakamani hapo, shahidi huyo aliukana na kudai kuwa ni wa kugushi muhtasari wa kikao ambao unaonyesha yeye ni mmoja wa washiriki, jambo ambalo alilipinga.
Kikao hicho ndicho kinachodaiwa kubadilisha watia saini katika akaunti za benki za TFF, jambo linalodaiwa kuwa lilifungua milango ya ufujaji na ubadhilifu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |