Zlatan Ibrahimovic amepata kadi nyekundu ya kwanza tangu ajiunge na klabu ya LA Galaxy, baada ya kumpiga kofi mchezaji wa timu ya Montreal wakati wa mechi ya ligi kuu ya Marekani MLS, tukio ambalo lilibainika kwa ushahidi wa picha za video.
Ibra alimpiga Michael Petrasso kufuatia mchezaji huyo kumkanyaga wakati wa harakati za uwanjani, ambapo Petrasso pia alipewa kadi ya njano.
Ibrahimovic amefunga magoli matatu kwenye mechi saba alizocheza tangu ajiunge na ligi hiyo mwezi machi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |