Mtaalam kutoka Ethiopia amesema China bado inapaswa kuchukuliwa kama nchi inayoendelea licha ya juhudi zake za kupunguza umasikini katika miongo iliyopita.
Mkurugenzi wa Kituo cha Kimataifa cha Ushauri Gedion Jalata amesema, madai yanayotolewa na baadhi ya maofisa na wataalam wa nchi za Magharibi kuwa China inapaswa kuchukuliwa kama nchi iliyoendelea sio sahihi. Amesema Benki ya Dunia imeiweka China kama nchi inayoendelea kwa kufuata GDP, ingawa China imekuwa nchi ya pili kwa ukubwa kiuchumi duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |