Mamlaka hiyo imetolewa na Waziri wa Michezo wa Tanzania, Harrison Mwakyembe, baada ya mwenyekiti wa kamati ya kusimamia mchezo wa ngumi nchini Tanzania, kueleza kuwa wanashindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na vikwazo walivyowekewa na viongozi hao wa TPBO na PST, ambao ni Yassin Abdallah, na Emmanuel Mlundwa.
Zaidi waziri Mwakyembe amesema serikali imesikitishwa na taarifa kuwa viongozi hao wamekuwa wakifanya vurugu, na wakati mwingine kuidhihaki serikali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |