Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Southgate amemteua mchezaji wa klabu ya Tottenham Harry Kane kuwa nahodha wa kikosi kitakachoshiriki mahsindano ya kombe la dunia mwezi ujao.
Uamuzi wa kocha huyo kumteua Kane, umekuja kutokana na alichodai kuwa ni juhudi alizozionyesha mchezaji huyo kila wakati alipoitwa kuitumikia timu ya taifa, lakini pia kutokana na mwenendo wake kwenye ligi kuu ya uingereza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |