• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda yapewa ushirika rasmi wa matangazo ya mauzo ya Arsenal

    (GMT+08:00) 2018-05-24 19:42:56
    Rwanda imeteuliwa kuwa mshirika rasmi wa klabu ya soka ya Uingereza ya Arsenal na sasa klabu hiyo itaonekana na nembo ya Visit Rwanda kwenye jezi zao.

    Rais Paul Kagame amesema yeye kama shabiki wa klabu hiyo amefurahishwa na hatua hiyo .

    Kagame amesema nembo hiyo itatumika kuvutia watalii Rwanda pamoja na wawekezaji wa kibiashara.

    Afisa mkuu wa mauzo ya Arsenal Vinai Ventkatesham amesema wamechagua kushirikiana na nchi hiyo baada ya kurishishwa na mabadiliko ya maendeleo yake tangu tukio la vita.

    Jezi ya Arsenal inatazamwa na watu milioni 35 kwa siku duniani na ni moja ya timu zinazopendwa sana na mashabiki.

    Bodi ya maendeleo ya Rwanda imearifu kwamba Rwanda itaendelea kukuwa kiuchumi kutokana na mradi huo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako