Waziri wa afya wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC Bw. Oly Ilunga amesema mpaka sasa jumla ya watu 52 wanaoshukiwa kuambukizwa homa ya Ebola wameripotiwa, na 31 kati yao wamethibitishwa. Kwa mujibu wa Wizara ya afya ya DRC, mgonjwa mwingine wa Ebola ameripotiwa kufariki jana kwenye eneo la Bikoro mkoani Ikweta, kusini magharibi mwa DRC, wakati chanjo ya homa hiyo inaendelea kutolewa kwenye eneo hilo kuanzia Jumatatu wiki hii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |