Watu wasiopungua 49 wamefariki dunia baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika Mto Kongo, kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC.
Gavana wa mkoa wa Tshuapa Bw. Mboyo Iluka amesema boti hiyo iliyokuwa ikisafiri kutoka kijiji cha Monkoto kuelekea Mbandaka imezama na chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.
Tume inayoundwa na maofisa waandamizi wa mkoa huo imepelekwa kwenye eneo la ajali kuchunguza chanzo cha ajali hiyo.
Ajali katika Mto Congo huwa zinasababishwa na hali mbaya za boti au boti kubeba abiria kupita kiasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |