• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yapinga uchokozi wa Marekani kwenye bahari yake

    (GMT+08:00) 2018-05-28 09:58:59

    China imepinga vikali manowari mbili za Marekani kuingia kwenye eneo la bahari ya China karibu na Visiwa vya Xisha.

    Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Lu Kang amesema manowari za Marekani ziliingia jana usiku kwenye eneo la bahari ya China karibu na Visiwa vya Xisha bila ruhusa ya serikali ya China. Jeshi la majini la China lilizitambua, kuzionya na kuzifukuza.

    Bw. Lu Kang amesema visiwa vya Xisha siku zote ni ardhi ya China, na serikali ya China ilitangaza mpaka wa eneo la majini la Visiwa vya Xisha mwaka 1996.

    Pia amesema kitendo hicho cha manowari za Marekani, kimekwenda kinyume cha sheria za China na za kimataifa, na kimeingilia vikali mamlaka ya China, na kuhatarisha amani, usalama na utaratibu kwenye maeneo husika ya bahari.

    Pia amesisitiza kuwa China itachukua hatua zote za lazima kulinda mamlaka na usalama wake. Wizara ya Ulinzi ya China pia imepinga vikali kitendo hicho cha Marekani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako