Kocha mkuu wa Rayon Sport inayoshiriki ligi kuu nchini Rwanda, Ivan Minneart amesema amewaambia vijana wake endapo watahitaji kushinda kutetea ubingwa ni lazima washinde mechi zote 10 walizosaliwa nazo katika msimu huu.
Mpaka sasa timu hiyo imecheza mechi 20, na iko katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi baada ya kujikusanyia pointi 37, ikizidiwa kwa pointi 13 na vinara APR.
Timu hiyo leo inacheza dhidi ya Miroplast FC kwenye uwanja wa Kigali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |