Wizara ya Usafiri imesema shilingi inaendelea kudhoofika kutokana na matumizi makubwa ya mafuta na magari ya zamani.
Asilimia kubwa ya magari nchini Uganda ni ya zamani sana, na hutumia mafuta mengi ikilinganishwa na mpya. Fedha nyingi za kigeni kisha huenda katika kuagiza mafuta
Wizara hiyo, imesema kuna haja ya Uganda kuhamasisha kuagizaji wa magari mapya ili kupunguza matumizi ya mafuta.
Bw Bagonza, ambaye aliwakilisha waziri wa Ujenzi, katika uzinduzi wa malori ya Monkey Man huko Kampala amesema sekta ya lori nchini Uganda inajulikana kwa magari ya zamani, ambayo si tu madhara kwa mazingira lakini pia uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |