Serikali ya Ethiopia imefutilia mbali leseni za baadhi ya kampuni za kuchimba dhahabu katika eneo la Guji wilaya ya Oromia .
Hii ni kufuatia malalamishi ya wananchi kuhusu uharibifu wa mazingira na maji .
Bacha Faji ni msemaji wa wizara ya petrol na gesi , aliesisitiza kwamba kampuni zinazofanya sghuhuli ya uchimbaji zimekataa kushirikiana na serikali katika tuhuma za uharibifu huo.
Kampuni hiyo kutoka Saudi Arabia zimepokonywa leseni na kutakiwa kusimamisha kazi hiyo hadi pale muafaka utakapopatikana.
Utafiti unaonyesha kwamba eneo la Guja linatoa zaidi ya tani 4.5 ya dhahabu kwa mwaka
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |