Kundi la Islamic State limetangaza kuwajibika na shambulizi lililotokea Jumanne dhidi ya mjini Liege nchini Ubelgiji, na kusababisha vifo vya watu wanne. Shirika la habari la Amaq News lenye uhusiano na kundi hilo, limesema mshambuliaji ambaye ni askari wa kundi la IS aliwaua maofisa wawili wa polisi na raia mmoja, na kuwajeruhi polisi wengine wanne, kabla ya kuuawa kwa kupigwa risasi na polisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |