• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • WHO yawatahadharisha watalii wa kimataifa kuhusu mlipuko wa Ebola DRC

    (GMT+08:00) 2018-05-31 09:51:22

    Shirika la afya duniani WHO limewatahadharisha watalii wa kimataifa kuhusu mlipuko wa Ebola nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo DRC kutokana na mwelekeo mpya wa homa hiyo.

    Shirika hilo limesema kwa ujumla hatari ya maambukizi ya homa ya Ebola kwa watalii nchini DRC ni ndogo, kwa kuwa wagonjwa wanaweza kuambukiza wengine baada ya kuonesha dalili ikiwa ni pamoja na homa, kukosa nguvu, maumivu ya misuli, kichwa na koo.

    WHO imewashauri watalii wanaotaka kwenda DRC kutafuta ushauri wa kidaktari zaidi ya wiki nne hadi nane kabla ya safari. Ushauri huo, ni pamoja na hatari za kiafya, mahitaji ya chanjo na dawa za malaria, pamoja na vitu vingine vya matibabu vinavyohitajika.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako