Korea Kusini imeidhinisha ziara ya mtawa wa Kibudha kwenda Korea Kaskazini, ikiwa ni idhinisho la kwanza kwa mawasiliano ya kiraia kati ya nchi hizo mbili chini ya serikali ya rais Moon Jae-in.
Mtawa huyo, Ven. Cheondam, ambaye pia ni mkuu wa Jumuiya ya Amani ya Dunia, anatarajiwa kufanya ziara nchini Korea Kaskazini kuanzia Juni 2 hadi 6. Akiwa nchini humo, mtawa huyo atakutana na mwenzake wa Korea Kaskazini ili kujadiliana kuhusu kukarabati hekalu lililopo Mlima Kumgang, kusini mashariki mwa nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |