Wizara ya mazingira na ikolojia ya China leo imetoa ripoti ya hali ya mazingira na ikolojia ya China katika mwaka 2017, ikionesha kuwa kiwango cha hali ya hewa na mazingira ya maji cha China kimeboreshwa katika mwaka 2017, na hali ya mazingira ilikuwa na utulivu.
Mkurugenzi mkuu wa idara ya usimamizi wa mazingira ya wizara hiyo Bw. Liu Zhiquan amesema, miongoni mwa miji 338 nchini China, hali ya hewa na mazingira katika miji 99 imefikia kiwango cha ubora, ambayo imechukua asilimia 29.3.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |