Aliyekuwa mwanariadha bingwa wa olimpiki Usain Bolt anaendelea na nia yake kusaka nafasi ya kucheza soka, na sasa matarajio yake ni kuiwakilisha timu yake ya taifa kwenye mechi dhidi ya timu ya taifa ya Norway ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 19. Jana alionekana akifanya mazoezi na timu moja ya daraja la kwanza ya Norway, ikiwa ni sehemu ya mazoezi yake ambapo pia anatarajiwa kuichezea timu ya dunia dhidi ya timu ya wasanii nyota wa Uingereza, kwenye mechi ya hisani itakayochezwa katika uwanja wa Old Trafford juni 10.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |