Soko la hisa la China limewekwa rasmi kwenye masoko yanayoinuka ya MSCI usiku wa manane wa tarehe 31 Mei.
Msemaji wa Shirikisho la usimamizi wa hisa la China Bw. Chang Depeng leo hapa Beijing amesema, hii ni hatua muhimu katika mchakato wa kimataifa kwa soko la hisa la China. Pia ni chaguo la busara la wawekezaji duniani kutokana na wimbi la maendeleo, na ni matokeo ya lazima ya ujenzi wa utandawazi wa kimataifa kwa soko la hisa la China.
Bw. Chang amesema, ukweli wa maendeleo ya soko la hisa la China umeonesha kuwa, China lazima ishikilie mageuzi na kufungua mlango kwa nje, ili kuinua uwezo wa kuhudumia uchumi halisi kwa soko la hisa, na kuongeza nguvu ya ushindani ya soko la hisa la China duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |