Mradi mpya wenye lengo la kushughulikia changamoto za mataifa maskini duniani kimezinduliwa rasmi mjini Gebze nchini Uturuki.
Mradi huo kwa jina "Benki ya Teknolojia", utashughulikia matatizo ya nchi hizo maskini kupitia sayansi, teknolojia pamoja na ubunifu.
Akihutubia wakati wa uzinduzi wa mradi huoo ,Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bi Amina Mohammed, amesema uzinduzi huo ni wa muhimu katika kusaidia mataifa yaliyo na maendeleo duni -LDCs kuweza kujiendeleza kwa kutumia faida za sayansi, teknolojia na ubunifu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |