Andy Murray wa Uingereza ameongezewa muda wa kupumzika baada ya matibabu aliyopata mwezi Januari kutokana na majeraha kwenye misuli ya mapaja, jambo lililomfanya asishiriki mashindano yoyote tangu kuanza kwa mwaka huu.
Kutokana na hilo, Murray amelazimika kujiondoa kwenye mashindano ya Uholanzi yatakayoanza Juni 11.
Licha ya hali hiyo, mchezaji huyo ambaye ni namba moja kwa ubora nchini Uingereza, bado ana matumaini ya kushiriki mashindano ya Wimbledon yatakayofanyika mwezi julai jijini London.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |