Watu karibu mia mbili bado hawajulikani walipo kufuatia mlipuko wa volkano ya Fuego nchini Guatemala.
Kwa mujibu wa takwimu mpya kutoka Taasisi ya Taifa ya Sayansi Misitu ya Guatemala, idadi ya vifo vilivyotokana na mlipuko huo imefikia 75.
Volcano ya Fuego ililipuka Jumapili mchana na baadaye uji wa volcano hiyo ukaanza kusambaa. Idara ya Udhibiti wa Maafa ya nchi hiyo imesema huu ni mlipuko mkubwa zaidi ulioshuhudiwa katika miaka ya hivi karibuni.
.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |