Askari watano wa jeshi la polisi nchini Kenya wameuawa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga bomu lililotegwa kando ya barabara katika mji wa mpaka kati ya nchi hiyo na Somalia leo asubuhi.
Kamishna wa polisi wa kaunti ya Kirinyaga Joshua Chepchieng amethibitisha tukio hilo, akisema askari polisi hao walikuwa wakielekea kwenye kituo cha mpakani cha Liboi wakati gari lao lilipokanyaga bomu hilo.
Hakuna kundi lolote lililokiri kuhusika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |