Kazi ya kutafuta ndege iliyopotea Jumanne katikati ya Kenya imesitishwa kwa mara ya pili kutokana na hali mbaya ya hewa.
Kamishna wa kaunti ya Nyandarua Bw. Boaz Cherutich amesema kazi ya utafutaji imesitishwa kutokana na hali mbaya ya hewa katika msitu wa Aberdares ambako ndege inadhaniwa kuanguka.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Fly-SAX, ilikuwa na abiria 8 na wafanyakazi 2, na ilipoteza mawasiliano na mnara wa kuongozea ndege jumanne mchana wakati ikitoka Kitale kwenda Nairobi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |