Idara ya upelelezi ya Rwanda RIB imesema, maofisa wasiopungua watano wa serikali za mitaa za Rwanda wamekamatwa kutokana na udokozi wa fedha za umma, upendeleo na matumizi mabaya ya mali.
Maofisa hayo waliokamatwa na RIB ni pamoja na naibu meya wa wilaya ya Burera kaskazini mwa Rwanda anayeshughulikia mambo ya uchumi, katibu mtendaji wa wilaya hiyo, meya wa zamani na naibu meya wa zamani.
RIB pia inawataka wananchi watoe habari kuhusu vitendo vya udokozi wa fedha za umma.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |