Mwamuzi wa Kenya aliyetueuliwa kucheza fainali za kombe la dunia nchini Russia, Aden Marwa, ameondolewa kwenye fainali hizo baada ya kugunduliwa kuwa alipokea rushwa ya dola 600 kutoka kwa mwandishi wa habari wa Ghana Anas Aremeyaw. Marwa amekuwa mmoja wa wahanga wa kashfa ya ufsadi ya shirikisho la soka Afrika CAF lililofichuliwa na mwandishi wa habari wa Ghana, na kuwanasa maofisa kadhaa wakipokea milungula.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |