Mkurugenzi wa Shirika la nishati ya atomiki la Iran Bw. Ali Akbar Salehi amesema nchi yake imefanya maandalizi ya kujenga mifumo wa msukumo wa nishati ya nyuklia. Amesema mradi huo ni mkubwa na itachukua muda kuukamilisha, na sasa bado wako kwenye kipindi cha maandalizi, na wataalamu wengi wa shirika hilo wameshiriki kwenye utafiti wa mifumo itakayotumiwa kwenye usafiri baharini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |