Waziri wa Fedha ameahidi kushughulikia hali hiyo kabla ya mwisho wa Ramadan.
Hata hivyo, Wanauchumi wanashutumu sana Sheria ya sasa ya Udhibiti wa Mambo ya Nje iliyopitishwa hivi karibuni.
Ukosefu wa fedha taslimu nchini Sudan, ulipelekea kufungwa kwa vituo vya kutoa fedha maarufu kama ATM.
Waziri aidha amesema kuongezeka kwa madeni ya nje ya nchi pia inachangia ukosefu wa fedha nchini.
Uchumi wa Sudan unakabiliwa na matatizo makubwa na madeni ya kigeni zaidi ya dola bilioni 50.
Waziri alitoa kiwango cha mfumuko wa bei wa asilimia 54.1 katika robo ya kwanza ya mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |