• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Kukuza bishara ya EAC, lazima ushuru ipunguzwe

    (GMT+08:00) 2018-06-11 20:30:44
    Waziri wa Maendeleo ya Afrika Mashariki na Ushoroba wa Kaskazini Peter Munya amesema utozaji wa ushuru mara mbili itakatiza ukuaji wa soko la uchumi wa Afrika Mashariki.

    Munya amezitaka serikali za kaunti kuacha kutoza ushuru mara mbili kwa malori yaliyo kwenye safari, ni kinyume na katiba .

    Munya alikuwa akizungumza Kitale wakati wa warsha ya kuhamasisha kwa Wanachama wa kaunti.

    Pia ameomba kaunti kupunguza vikwazo vya barabara ambavyo vinazuia usafirishaji wa bidhaa kutoka bandari ya Mombasa kwenda nchi nyingine za Afrika Mashariki.

    amesema Kenya inapoteza biashara yake ya kikanda kwa nchi jirani kwa sababu ya changamoto zinazozuia usafirishaji wa haraka wa bidhaa.

    Mauzo ya nje ya Kenya imefikia asilimia 25 ya bidhaa na huduma kwa nchi za Afrika Mashariki na hii imebakia soko muhimu zaidi kwa mauzo ya nje ya Kenya.

    Katibu wa kudumu Susan Koech amesema serikali itasaidia wilaya za mpaka ili kuhakikisha kuwa maono ya Jumuiya ya Afrika Mashirika EAC yameonekana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako