• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ubeligiji yashinda 4-1 dhidi ya Costa Rica

    (GMT+08:00) 2018-06-12 09:20:33

    Katika moja ya mechi za kirafiki zilizopigwa jana, mchezaji Romelu Lukaku ameifunga magoli 2 katika ushindi wa 4-1 iliopata timu ya taifa ya Ubeligiji ilipocheza dhidi ya Costa Rica mjini Brussels.

    Costa Rica walikuwa wa kwanza kupata goli kupitia Bryan Ruiz katika dakika ya 24, kabla ya Dries Mertens kusawazisha katika dakika ya 31.

    Lukaku alifunga magoli mawili mfululizo katika dakika za 42 na 50 na kuifanya timu yake iongoze kwa magoli 3-1 na baadaye Michy Batshuayi akifunga la mwisho kunako dakika ya 64.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako