Wasanii Robbie Williams na Aida Garifullina ndiyo watakaotumbuiza katika siku ya ufunguzi wa michuano ya kombe la dunia ya mwaka huu, kwenye hafla itakayofanyika kwenye uwanja wa Luzhniki mjini Moscow siku ya Alhamisi.
Pamoja na wasanii hao, kwa mujibu wa FIFA sherehe hizo pia zitahusisha wegine wazawa.
Lakini umoja wa wanasoka wa zamani utawakilishwa na Ronaldo De Lima wa Brazil ambaye atakuwa jukwaa kuu.
Sherehe hizo za ufunguzi zitaanza rasmi majira ya saa 12 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |