• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yavutia uwekezaji wa China kwenye uzalishaji viwandani

    (GMT+08:00) 2018-06-13 09:35:54

    Serikali ya Kenya imetangaza mpango wa kuvutia zaidi uwekezaji wa China kwenye sekta ya uzalishaji viwandani. Ofisa wa Wizara ya viwanda ya Kenya Bw. Adan Mohamed ameliambia baraza la biashara mjini Nairobi, kuwa Kenya imetangaza motisha mbalimbali ikiwa ni pamoja na wa kifedha na hata miundombinu ili kuifanya nchi hiyo iwe na gharama ndogo za uzalishaji.

    Kwenye baraza hilo lililopewa jina la Guangzhou-Foshan-Nairobi, Kenya pia imetangaza kuwa inafikiria kuifanya sarafu ya China kuwa sarafu ya akiba. Gavana wa benki kuu ya Kenya Bw. Patrick Njoroge amesema nchi kadhaa za Afrika pia zinafikiria kuifanya sarafu ya China kuwa sarafu ya akiba.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako