Klabu ya Real Madrid wamemteua kocha mkuu wa timu ya taifa ya Hispania Julien Lopetegui kuwa kocha wake kwa mkataba wa miaka mitatu.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 51 atachukua wadhfa huo ulioachwa wazi na Zinedine Zidane ambaye alisema klabu hiyo inahitaji sauti mpya, na sasa Lopetegui ataanza rasmi kazi baada ya michunao ya kombe la dunia.
Kabla ya kuchukua jukumu la kuifundisha timu ya taifa ya Hispania, Lopetegui alikuwa kocha mkuu wa klabu ya FC Porto ya Ureno kwa miaka miwili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |