Waziri mkuu wa Iraq Bw. Haider al-Abadi ametoa wito kwa vyama vya kisiasa nchini humo kukutana baada ya sikukuu ya Eid el-Fitr, kwa lengo la kufikia mwafaka kuhusu taratibu mpya za kuunda bunge na serikali ijayo. Wito huo umetolewa wakati mvutano wa kisiasa unapamba moto kutokana na tuhuma za kuwepo kwa vitendo vya udanganyifu na ukiukaji kanuni kwenye uchaguzi wa bunge uliofanyika Mei 12.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |