Baraza la mahakama ya waislamu la Afrika Kusini (MJC) limelaani vikali shambulizi la kikatili lililotokea jana karibu na mji wa Cape Town, na kusababisha vifo vya waumini wawili wa kiislamu na wengine wawili kujeruhiwa.
Baraza hilo limesema mtu asiyejulikana aliingia msikitini na kujiunga na waumini kwenye sala ya usiku, baadaye alimvamia Imam na kumchoma kisu, na kuwachoma visu watu waliokwenda kumsaidia Imam huyo. Imam aliyeshambuliwa na mshambuliaji wote ni wasomali.
Kamishna mkuu wa Polisi Bw Khehla Sitite ameiambia kamati ya usalama ya bunge, kuwa polisi na idara ya upelelezi wameanza uchunguzi kuhusu tukio hilo na wamelipa kipaumbele.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |