Kamati ya afya ya taifa ya China imesema China itaendelea na juhudi za kuhamasisha umma kuchangia damu na kutarajia kuwa na wachangia damu 15 kati ya kila watu elfu moja ifikapo mwaka 2020. Ofisa wa kamati hiyo Bw. Zhou Changqiang amesema ifikapo mwaka 2020 damu yote itakayotumiwa kwa ajili ya matibabu itakuwa imechangiwa, na kwamba kamati hiyo itaanzisha kampeni ya uchangiaji damu kuanzia Julai hadi Septemba mwaka huu wakati China inaadhimisha miaka 20 ya sheria ya uchangiaji damu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |