Baraza la usalama la Umoja wa mataifa limekaribisha uamuzi wa serikali ya Afghanistan wa kurefusha usitishwaji vita wa muda na kundi la Taliban baada ya sikukuu ya Eid el-Fitr. Taarifa iliyotolewa na baraza hilo inasema wajumbe wa baraza hilo wameeleza masikitiko yao makubwa kuwa kundi la Taliban halijarefusha muda wa usitishaji vita huo, na kuwahimiza waitikie uamuzi wa serikali, na pia wamesisitiza wito wao wa kundi la Taliban kukubali mwaliko uliotolewa mwezi Februari na serikali ya Afghanistan, kushiriki kwenye mazungumzo ya amani bila masharti.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |