Katika mechi tatu zilizopigwa jana, Timu ya taifa ya Ubeligiji ilipata ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Panama, Uingereza ikaifunga Tunisia kwa magoli 2-1 na Sweden ikapata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Korea Kusini.
Michuano hiyo inaendelea tena leo kwa mechi tatu, mbili za kundi H ambapo Colombia itacheza na Japan, Senegal ikicheza dhidi ya Poland, na wenyeji Urusi kutoka kundi A watacheza dhidi ya Misri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |