• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wizara ya Biashara ya China yatoa hotuba kufuatia tangazo lililotolewa na Ikulu ya Marekani tarehe 18, Juni

    (GMT+08:00) 2018-06-19 10:42:48
    Msemaji wa wizara ya biashara ya China amesema China italazimika kuchukua hatua madhubuti kujibu hatua ya ushuru ya Marekani iliyotishia kuongeza ushuru kwa bidhaa za China zenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 200, baada ya kutangaza kuongeza ushuru dhidi ya bidhaa za China zenye thamani ya dola bilioni 50.

    Wizara ya Biashara ya China imesema hatua inayochukuliwa na Marekani ya kuishinikiza na kuisaliti China, inaenda kinyume na makubaliano yaliyofikiwa kwenye mazungumzo mengi kati ya nchi hizo mbili, na pia imeisikitisha jumuiya ya kimataifa. Marekani kuanzisha vita ya kibiashara hakulingani na kanuni za soko wala mkondo wa maendeleo ya dunia wa sasa, pia kumeharibu maslahi ya watu na makampuni ya nchi hizo mbili, na wa dunia nzima.

    Wizara hiyo imeongeza kuwa China itachukua hatua zinazolingana na kitendo hicho cha Marekani, hii sio tu ni kwa ajili ya kulinda maslahi ya taifa na wananchi wa China, bali pia ni kulinda mfumo wa biashara huria na maslahi ya pamoja na binadamu. Bila kujali jinsi mazingira ya nje yanavyobadilika, China itafuata mpango wake, kutoa kipaumbele maslahi ya wananchi, kusukuma mbele mageuzi na ufunguaji mlango, kuhimiza ukuaji mzuri wa uchumi na kuongeza kasi ya kujenga mfumo wa uchumi wa kisasa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako